Thursday, July 31, 2014

SIRI 9 ZINAZOFANYA NDOA KUWA YENYE FURAHA.




Siri ya kudumisha ndoa yenye furaha ni pamoja na kumuoa au kuolewa na mtu ambaye ni rafiki yako. Kwa maana nyingine urafiki mwema hupelekea kuwa na ndoa yenye furaha baadaye. Mnaweza kuishi kama  marafiki  mkicheza na kufurahi kuwa pamoja muda wote. Msitegemee kuwa tendo la ndoa pekee ndilo lijenge ndoa yenu hapo mtakuwa mnajidanganya, fikiria kama ikitokea kwa bahati mbaya mmoja wenu akafanyiwa upasuaji utakao pelekea kutofanya tendo la ndoa je mtaendelea kuifurahia ndoa yenu au ndio mtaishia hapo?. Hakikisha hukati mawasiliano na mke au mume wako, likitokea jambo linalowakwaza, kaeni ninyi wawili mlimalize. Hakikisheni mnadumisha upendo wenu wa kwanza mlio anza nao. Kumbuka ndoa ni kitu kigumu kinahitaji kila mmoja kujitoa kikamilifu kwa mwenzake pamoja na kumuona mwenzake ni wamuhimu saana kwake. Hapa tutaangalia mambo mbalimbali yatakayopelekea wewe udumu kuwa a ndoa yenye furaha.
Siri za kuwa na ndoa yenye furaha.Ndoa ambayo itadumu kuwa na furaha katika muda wote wa maisha yao ni ile ambayo wanandoa wataelewana, wanasoma vitabu pamoja, wanahudhuria semina mbalimbali pamoja, watasoma machapisho mbalimbali yahusuyo ndoa kwenye mtandao pamoja na kuona mfano wa ndoa zingine ambazo zina mahusiano mema na kujifunza kwazo pamoja.
Yafuatayo ni mambo ambayo kama yakifuatwa na wanandoa kikamilifu yaweza kuwafanya wanandoa kuishi kwa furaha katika maisha yao ya ndoa.
1.  Usikate mawasiliano.
Kumbuka siku unakutana na mchumba wako kwa mara ya kwanza mlielewana kwa njia ya mawasiliano , hivyo bila mawasiliano mazuri na mke au mume wako fahamu kwamba ndoa yenu  iko kwenye matatizo. Kuongea pamoja, kuelezana pamoja kile ambacho kila mmoja anakihitaji katika maisha yenu ya ndoa huleta maelewano mema kati yenu. Ni kweli kwamba kadri ambavyo mnavyozidi kuishi pamoja mawasiliano yaweza kupungua kwa sababu ya kuzoeana saana lakini kamwe msiruhusu kabisa mawasiliano kukatika. Mawasiliano mema kati yenu ni muhimu katika kuelewa hitaji la mwenzako na huleta furaha katika mahusiano yenu.  Mawasiliano ni muhimu, tumia maneno mengi zaidi kuwasiliana na Yule uliyemchagua kuishi naye japo vitendo ni muhimu zaidi kama kumshika mkono, kumkumbatia, kumvalisha, kuvaa nguo wewe mwenyewe nguo nzuri, jipulizie pafumu ile ambayo mchumba wako anaipenda, mpe zawadi japo ni ndogo na za kawaida, vitu hivi huboresha saana mawasiliano ya wana ndoa.
2.  Sikilizaneni.
Masikilizano mema ni muhimu kwa afya ya ndoa yenu. Kuwa tayari muda wote kumsikiliza mwenzako. Baada ya ratiba ngumu za siku kuwa na hamu ya kumsikiliza mwenzako kwa kumuuliza maswali mbalimbali, lakini kumbuka- wakati mwingine hata mke au mume wako naye anahitaji kuku uliza au kukusikiliza, hivyo epuka saana kutoa hitimisho wewe tu!, fungua masikio yako na msikilize kile anachosema mwenzako.
3.  Ucheshi na ukweli.
Moja ya kitu muhimu saana katika kuwa na familia au ndoa bora ni ucheshi kwa wana ndoa. Ni vigumu saana kubaki na hali ya kufahi na kucheka pamoja lakini mnaweza kufanikiwa katika hili kwa kutembelea wote katika maeneo mapya kwa pamoja mkiwa wenyewe tu wewe na mume ama mke wako.
Kuwa muwazi na mkweni ni msingi muhimu saana kwa wanandoa, hakikisha unakuwa mkweli kwa mke au mume wako hiyo itawafanya  muaminiane wote na ndoa yenu itakuwa ni ya furaha siku zote.
4.  Onesha upendo.
Hakikisha unatumia muda mwingi kuongea na Yule umpendaye. Unaweza kuwa mbali na mume au mke wako lakini unaweza kumudu kuongea na umpendaye hata kwa njia ya simu, ili mradi tu onesha kuwa unampenda na kumjali.
Onesha unampenda saana mke au mume wako daima. Kila siku hakikisha unadhihirisha upendo wako kwake usichoke. Mbusu mke au mume wako, mkumbatie kila mara kama ishara ya upendo. Kama mtapendana kwa dhati basi bila shaka mtaheshimiana, na kila mmoja atamthamini mwenzake. kila siku tafakari kwa nini ulimpenda yeye tu na wala si mwingine, hii itakufanya umpende zaidi mke au mume wako.
5.  Mthamini mke au mume wako.
Ili kila mmoja awe na amani katika ndoa ni lazima kila mmoja awe na mchango sawa katika mahusiano. Usioneshe  kuwa wewe ni bora kuliko mwenzi wako hii ita mfanya mwenzako ajisikie hana uhuru. Hii ita hafifisha mahusiano yenu kama mke au mume.
6.  Furahi pamoja na mke au mume wako.
Kudumisha upendo kwa wanandoa ni rahisi tu, furahia kuwa pamoja na umpendaye, ongeeni pamoja, fanyeni mambo mbalimbali ya kifamilia pamoja na kwa upendo.Wakati watu wawili wanapoishi pamoja, ni lazima tu watu hawa watatofautiana kwa baadhi ya mambo kwa sababu binadamu wote tunatofautiana namna tunavyo fikiri na kutoa maamuzi. Wakati hali hii ya kutoelewana inapotokea kwa wana ndoa, tumieni hekima saana kumaliza tofauti hizo, ili kuacha upendo wenu uzidi kuwa imara na wala si dhaifu.
7.  Samehe na kusahau.
Wana ndoa wanaofanikiwa katika maisha yao ya ndoa ni wale wanao pokea na kutoa msamaha. Ni wale wanao samehe na kusahau kabisa makosa ya wapenzi wao. Wakati wanapofanya makosa ambayo yanawaumiza wapenzi wao wao wana omba msamaha. Hivyo kusameheana ni jambo la muhimu saana katika mahusiano.
8.  Kuvumiliana.
Wanandoa wanaofanikiwa kuishi muda mrefu wakiwa nafuraha daima ni walewanaovumilia hali zote za maisha. Mfano wakati wa magonjwa, wakati wa utajiri, wakati wa umaskini, wakati wa afya njema.  Kama wanandoa wataweza kuvumiliana katika hali zote hizi basi wataishi kwa furah kwa sababu watakuwa wamezipitia nyakati zote hizi, hivyo kila mmoja atamuona mwenzake ni muhimu zaidi.
9.  Muwazie mema mke au mume wako.
Ndoa nyingi zimekuwa zikifurahia maisha ya ndoa kwa sababu wote wanawaziana mema. Mhurumie umpendaye, mjali mtie nguvu pale ambapo anakata tama, weka upendo wako wote kwake.