This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

Thursday, July 31, 2014

SIRI AJABU ILIYOMO NDANI YA MAHUSIANO



Watu wengi wanapata uzoefu wa mapenzi kutoka kwenye maadili ya tamaduni mbalimbali zinazofahamika. Tunaamini kuwa mapenzi yanaweza kuleta mabadiliko makubwa kwenye maisha. Mtazamo wa kimapenzi unaotokana na tamaduni mbalimbali unajenga taswira ambazo sio sahihi, mitazamo yao ipo kwa ajili ya kuburudisha tu na wengi tunafikiria kuwa hayo ndiyo mapenzi. Mtu anapopenda mno kiasi cha kuwa na wazimu wa kimapenzi wengi huwa tunafikiria kuwa huo ndio upendo. Tatizo linalojitokeza ni kwamba tunapogusa dhana ya mapenzi ya dhati wengi wanakufa mioyo kwasababu kuna vitu vingi havipo kwenye maadili ya tamaduni zetu. Baadhi wanahitaji waone jinsi ya kupenda kulingana na maadili ya mapezi ya kweli. Inawezekana kabisa na sio kuwezekana tu lakini pia tunataka ubadilishe mtazamo wako wa kupenda. Hebu fuata mtiririko huu ili kupata kile unachokihitaji;- jinsi ya kupenda na kupendwa. • Tambua tofauti iliyopo kati ya tamaa na upendo. Tamaa ni hali ya kisaikolojia ambapo mtu anakuwa na upendo wa msisimko unaosababisha kuzalishwa kwa homoni za mwili, tamaa haidumu. • Mapenzi ni mbinu ya kujifunza, sio kitu kinachotokana na homoni au mhemko mtu mmoja alisema kuwa upendo ni”tendo la hiari” usipo jifunza jinsi ya kupenda ni dhahiri utaumizwa tu, hii ni kwasababu utakuwa huna uzoefu. • Jifunze mbinu za mawasiliano. Hii ndio njia pekee ya kukuza uamifu na ukaribu. Jinsi unavyozidi kuwasiliana na yule umpendae ndivyo unavyopunguza kiwango cha kuumizwa. Siku zote tofauti baina ya watu wawili huwa ipo, lakini kama mahusiano yanaenda sawasawa hizo tofauti zinamezwa, kitu muhimu ni kuzitambua tofauti zenu ili zisije zikavunja mahusiano yenu. Lazma utambue kuwa mwenzako anatoka wapi, yeye ni nani na pia uwe na uwezo wakujitambulisha kwake, zitambue tofauti zenu kwanza na kuzishughulikia ili kujenga mazingira yatakayokuwa salama kwa wote. • Usiweke mawazo yako kwenye vitu unavyopewa na mpenzi wako, na jinsi anavyokujali, angalia kuwa mpenzi wako nae anataka nini, unaweza kufanikisha hili endapo utajifunza jinsi ya kujali wengine. • Msaidie mtu mwingine. Mfadhaiko unamsababisha watu kujishughulisha na mambo yao binafsi hivyo hawajifunzi namna ya kupenda hivyo huumia pindi wanapoyaanza mapenzi. Unavyozidi kujali wengine ndivyo utakavyo jali mahusiano yako na mpenzi wako. • Uwe na uwezo wa kukusanya mawazo ya wegine ambao wako katika mahusiano, ukweli wanaokuambia kuhusu mapenzi yao unaweza ukawa ndio ukweli kuhusu mapenzi yenu pia, watu wenye mifadhaiko huwa wanaamini kuwa hakuna ukweli tofauti na mifadhaiko yao. • Weka wazi yaliyo moyoni mwako ambayo hujaridhishwa nayo. Kuhisi kukataliwa ndio mwanzo wa mfadhaiko. Tambua kuwa sauti iliyo moyoni mwako ina nguvu lakini sio sahihi, inakubidi useme kuwa mimi sijakataliwa na kama unaona kuna udhafu wowote jaribu kuuweka wazi kuliko kuweka dhana ya kukataliwa.

Siri 14 zitakazomfanya umpendaye kuwa na furaha siku zote- Kwa kumfanya akupendaye kukuhisi kila muda.



 Je mpenzi wako anahitaji kuwa na wewe muda wote? Tangu nigundue siri hii nimependwa mara mbili zaidi nilivyopendwa wakati wa uchumba. Naamini baada ya kugundua na wewe kama mimi hautaamini jinsi unavyopendwa…   Watu huwa na tabia yakuonyesha upendo wa juu sana kwa jinsi ya tofauti na wengine huonekana kama kutokufahamu nini humaanisha. Ingawa kila mtu hutakiwa kujua namna ya kuuyeyusha moyo wa mwenzi wake kwasababu ni hatua ya mwisho ya kumshawishi mwenzi wako.

Kwaaajili ya mke wako/rafiki yako wa kike.

1.     Umshtushe mke wako siku moja na mandari (mtoko). Panga mahali pa kukutania siku za wikiendi au siku yoyote ambapo mna siku ya mapumziko. Hakikisha kuwa hana ratiba yoyote nyingine zaidi ya hiyo. Ndipo unapomwambia kuwa aambatane na wewe mwende kwenye supermarket au kitu kifananacho na hiki. Mpe muda wa kujiandaa vizuri, muda wa kuingia kwenye gari, na munaweza kubeba hata vyakula laini ama vipoza njaa. Mpeleke mwenzi wako kwenye bustani nzuuri maarufu kama beach na mwambie kuwa unampenda na ndiyo maana umeeandaa hili tukio ili kumdhihirishia ni jinsi gani unampenda.

2. Mwandikie mashairi. Na kama hii sio hobi yako pia zipo sehemu nyingi zenye mvuto. Jaribu kumsomea kitabu cha mashahiri yenye ujumbe wa kumsifia, nyimbo za upendo n.k. usirudie neno lolote kwasababu itazoeleka na atakudharau.

3.  Mpikie chakula kizuri na kitamu, washa mishumaa punguza mwanga wa taa na safisha nyumba. Na atakapofika nyumbani atakosa cha kusema.

4. Shika mkono wake kila mara mnapokwenda mahali popote nje na nyumbani. Kama hili haliwezekani {kwasababu mmoja wenu amebeba mototo} hakikisha unaendeleza mawasiliano ya nje. Hii itamfanya ajisikie kuwa unajivunia ukiwa nae na kamwe huwezi kumuacha.

5. Panga ratiba ya kupiga picha. Mpe nafasi mke wako ama rafiki wako wa kike ajipambe kwaajili yako, pia chukua picha zake ambazo utaweka kwenye pochi yako, ofisini ama kwenye gari lako. Mwambie kwamba yeye ni mzuri na kuwa amepiga picha nzuri.

6. Pata muda mchache wa kwake siku moja na umwandikie neno rahisi tu “Nakupenda”  na bandika popote pale. Bandika hilo neno bafuni kwenye kioo ama sehemu ambao kwa haikka ataona huo ujumbe. Hii huimarisha na kumfanya yeye kuwa wa pekee sana kwako na kukupenda sana. Na kama unahitaji kupanua wazo hili unaweza kumuachia ujumbe mtamu katika maeneo yake machache pale unapotoka.

7. Kama wewe ni mchoraji unaweza ukapata hamasa na kuchora Titanic, ukapaka rangi ama kumchora umpendaye. Utapata majibu mazuri kama amani yako imeimarishwa na kama bado mwambie kwamba huwezi kuumba kitu kizuri sana kama wewe.

Kwa mume wako/rafiki yako wa kiume.

1.     Baada ya kazi ngumu za wiki, mwandikie ujumbe mzuri sana wa kurudi nyumbani. Mtumie ujumbe wa upendo wa kumsihi aje nyumbani na pia wa kumkumbusha kuwa ni muda mwafaka wa kupumzika na wewe.

2. Vaa nguo za chumbani huku ukimsubiri atoke kazini. Hii itamfanya kukupenda zaidi. Na kwa hakika atakubali jitahada zako na itamuongezea upendo kwako.

3. Kama mwezi wako anarekebisha uso wake kama kunyoa ndevu, mfanyie hilo. Weka nyimbo za upendo kwa taratibu na kwa upole mnyoe. Wewe chukua muda wako na fanya hivi atajisikia kuwa anapendwa na anajaliwa.

4. Chukua muda wako mkiangaliana machoni. Kubali na tambua uwepo wake, tambua marashi na manukato yake na joto lake. Na kama unajisikia hata kumbusu fanya hivo.

5. Jifanye kumuhitaji. Mwanaume hutamani kuonekana kuwa yeye pekee ndiye anayekulinda, hivyo mwambie kuwa hujisikii vizuri na huwa unakuwa mpweke pale anapokosekana ama unajisikia vizuri na kuwa na amani pale anapokuwepo.

6. Mkumbatie kwa ghafla. Onyo-fanya hivi pale ambapo mpo wawili tu ili kwamba asije akajisikia kuwa hayuko huru au amelazimishwa. Napendekeza fanya hivyo kwa muda wa dakika 5-6 afu mpe nafasi.

7.Mnunulie tiketi ya mpira wa miguu au mpira wa kikapu ule ambao yeye angependa kuuona. Ili kuonyesha upendo nenda nae mkashabikie timu yake kwa pamoja.


SIRI 9 ZINAZOFANYA NDOA KUWA YENYE FURAHA.




Siri ya kudumisha ndoa yenye furaha ni pamoja na kumuoa au kuolewa na mtu ambaye ni rafiki yako. Kwa maana nyingine urafiki mwema hupelekea kuwa na ndoa yenye furaha baadaye. Mnaweza kuishi kama  marafiki  mkicheza na kufurahi kuwa pamoja muda wote. Msitegemee kuwa tendo la ndoa pekee ndilo lijenge ndoa yenu hapo mtakuwa mnajidanganya, fikiria kama ikitokea kwa bahati mbaya mmoja wenu akafanyiwa upasuaji utakao pelekea kutofanya tendo la ndoa je mtaendelea kuifurahia ndoa yenu au ndio mtaishia hapo?. Hakikisha hukati mawasiliano na mke au mume wako, likitokea jambo linalowakwaza, kaeni ninyi wawili mlimalize. Hakikisheni mnadumisha upendo wenu wa kwanza mlio anza nao. Kumbuka ndoa ni kitu kigumu kinahitaji kila mmoja kujitoa kikamilifu kwa mwenzake pamoja na kumuona mwenzake ni wamuhimu saana kwake. Hapa tutaangalia mambo mbalimbali yatakayopelekea wewe udumu kuwa a ndoa yenye furaha.
Siri za kuwa na ndoa yenye furaha.Ndoa ambayo itadumu kuwa na furaha katika muda wote wa maisha yao ni ile ambayo wanandoa wataelewana, wanasoma vitabu pamoja, wanahudhuria semina mbalimbali pamoja, watasoma machapisho mbalimbali yahusuyo ndoa kwenye mtandao pamoja na kuona mfano wa ndoa zingine ambazo zina mahusiano mema na kujifunza kwazo pamoja.
Yafuatayo ni mambo ambayo kama yakifuatwa na wanandoa kikamilifu yaweza kuwafanya wanandoa kuishi kwa furaha katika maisha yao ya ndoa.
1.  Usikate mawasiliano.
Kumbuka siku unakutana na mchumba wako kwa mara ya kwanza mlielewana kwa njia ya mawasiliano , hivyo bila mawasiliano mazuri na mke au mume wako fahamu kwamba ndoa yenu  iko kwenye matatizo. Kuongea pamoja, kuelezana pamoja kile ambacho kila mmoja anakihitaji katika maisha yenu ya ndoa huleta maelewano mema kati yenu. Ni kweli kwamba kadri ambavyo mnavyozidi kuishi pamoja mawasiliano yaweza kupungua kwa sababu ya kuzoeana saana lakini kamwe msiruhusu kabisa mawasiliano kukatika. Mawasiliano mema kati yenu ni muhimu katika kuelewa hitaji la mwenzako na huleta furaha katika mahusiano yenu.  Mawasiliano ni muhimu, tumia maneno mengi zaidi kuwasiliana na Yule uliyemchagua kuishi naye japo vitendo ni muhimu zaidi kama kumshika mkono, kumkumbatia, kumvalisha, kuvaa nguo wewe mwenyewe nguo nzuri, jipulizie pafumu ile ambayo mchumba wako anaipenda, mpe zawadi japo ni ndogo na za kawaida, vitu hivi huboresha saana mawasiliano ya wana ndoa.
2.  Sikilizaneni.
Masikilizano mema ni muhimu kwa afya ya ndoa yenu. Kuwa tayari muda wote kumsikiliza mwenzako. Baada ya ratiba ngumu za siku kuwa na hamu ya kumsikiliza mwenzako kwa kumuuliza maswali mbalimbali, lakini kumbuka- wakati mwingine hata mke au mume wako naye anahitaji kuku uliza au kukusikiliza, hivyo epuka saana kutoa hitimisho wewe tu!, fungua masikio yako na msikilize kile anachosema mwenzako.
3.  Ucheshi na ukweli.
Moja ya kitu muhimu saana katika kuwa na familia au ndoa bora ni ucheshi kwa wana ndoa. Ni vigumu saana kubaki na hali ya kufahi na kucheka pamoja lakini mnaweza kufanikiwa katika hili kwa kutembelea wote katika maeneo mapya kwa pamoja mkiwa wenyewe tu wewe na mume ama mke wako.
Kuwa muwazi na mkweni ni msingi muhimu saana kwa wanandoa, hakikisha unakuwa mkweli kwa mke au mume wako hiyo itawafanya  muaminiane wote na ndoa yenu itakuwa ni ya furaha siku zote.
4.  Onesha upendo.
Hakikisha unatumia muda mwingi kuongea na Yule umpendaye. Unaweza kuwa mbali na mume au mke wako lakini unaweza kumudu kuongea na umpendaye hata kwa njia ya simu, ili mradi tu onesha kuwa unampenda na kumjali.
Onesha unampenda saana mke au mume wako daima. Kila siku hakikisha unadhihirisha upendo wako kwake usichoke. Mbusu mke au mume wako, mkumbatie kila mara kama ishara ya upendo. Kama mtapendana kwa dhati basi bila shaka mtaheshimiana, na kila mmoja atamthamini mwenzake. kila siku tafakari kwa nini ulimpenda yeye tu na wala si mwingine, hii itakufanya umpende zaidi mke au mume wako.
5.  Mthamini mke au mume wako.
Ili kila mmoja awe na amani katika ndoa ni lazima kila mmoja awe na mchango sawa katika mahusiano. Usioneshe  kuwa wewe ni bora kuliko mwenzi wako hii ita mfanya mwenzako ajisikie hana uhuru. Hii ita hafifisha mahusiano yenu kama mke au mume.
6.  Furahi pamoja na mke au mume wako.
Kudumisha upendo kwa wanandoa ni rahisi tu, furahia kuwa pamoja na umpendaye, ongeeni pamoja, fanyeni mambo mbalimbali ya kifamilia pamoja na kwa upendo.Wakati watu wawili wanapoishi pamoja, ni lazima tu watu hawa watatofautiana kwa baadhi ya mambo kwa sababu binadamu wote tunatofautiana namna tunavyo fikiri na kutoa maamuzi. Wakati hali hii ya kutoelewana inapotokea kwa wana ndoa, tumieni hekima saana kumaliza tofauti hizo, ili kuacha upendo wenu uzidi kuwa imara na wala si dhaifu.
7.  Samehe na kusahau.
Wana ndoa wanaofanikiwa katika maisha yao ya ndoa ni wale wanao pokea na kutoa msamaha. Ni wale wanao samehe na kusahau kabisa makosa ya wapenzi wao. Wakati wanapofanya makosa ambayo yanawaumiza wapenzi wao wao wana omba msamaha. Hivyo kusameheana ni jambo la muhimu saana katika mahusiano.
8.  Kuvumiliana.
Wanandoa wanaofanikiwa kuishi muda mrefu wakiwa nafuraha daima ni walewanaovumilia hali zote za maisha. Mfano wakati wa magonjwa, wakati wa utajiri, wakati wa umaskini, wakati wa afya njema.  Kama wanandoa wataweza kuvumiliana katika hali zote hizi basi wataishi kwa furah kwa sababu watakuwa wamezipitia nyakati zote hizi, hivyo kila mmoja atamuona mwenzake ni muhimu zaidi.
9.  Muwazie mema mke au mume wako.
Ndoa nyingi zimekuwa zikifurahia maisha ya ndoa kwa sababu wote wanawaziana mema. Mhurumie umpendaye, mjali mtie nguvu pale ambapo anakata tama, weka upendo wako wote kwake.


SIRI 6 ZA AJABU ZINAZOIMARISHA UHUSIANO.




Uajabu wa kitu ni vile kilivyo cha pekee na kinavyofanya kazi tofauti na vingine. Tangu nimegundua siri hizi mahusiano yangu na rafiki yangu wa kike yameimarika na kuwa na furaha siku ziongezekapo, nawe ukizitumia hakika yangu ni kwamba uhusiano utaimarika kwa namna ya ajabu. Ili kuwa na mahusiano yenye kufanikiwa ni lazima kujua unafanyaje ili uhusiano wenu uwe ni wa kudumu. Zifuatazo ndizo siri 6 muhimu za kuzingatia pale unapozigundua. 
1.     KUWA NA URAFIKI WA KUDUMU
Jiulize mwenyewe kuwa ni urafiki wa aina gani ulikuwa nao kwa rafiki yako, fikiria mambo ambayo yanakufanya kufarahi na marafiki wengine mbali na mwenzi wako kama vile utani ulio mzuri na mambo mengine. Pia ni vema kuyatumia hayo bila siri katika mahusiano yenu. Kama unataka rafiki mzuri pia unatakiwa kuwa rafiki mzuri.
2.     KUTANA NA MAHITAJI YA WATU.
Kwa uhusiano uliofanikiwa ni mahala pazuri ambapo mahitaji ya watu wawili hukutanishwa. Jaribu kujihoji nini ambacho mwenzi wako anahitaji ili kuwa tayari kumtimizia hitaji lake. Huenda kwa namna moja anataka sehemu laini ya kuangukia ama anahitaji bega zuri kwaajili ya kuwa mahali pake pa kulilia. Na hii haiitaji kujadiliana na kujua mahitaji ya mwenzi ama mchumba lakini tu jitahidi kugundua bila yeye kujua kuwa ni yapi mahitaji yake na umtimizie hata kama ni anapenda kuambiwa kuwa umependeza wewe fanya hivyo.
3.     JIWEKEE MALENGO.
“Amka kila siku asubuhi na kujiuliza, nini nitakachokifanya leo kipya? Hata ijapokuwa ni mambo madogo lakini yakiunganishwa kila siku yanaleta tofauti katika mahusiano. Tafuta sehemu iliyotulia kila siku na kufikiria kwa makini juu ya jambo gani jipya utalifanya na pia kuweka  malengo ya mahusiano yenu, unaweza  kumpigia mchumba wako masaa ya mchana kumsalimu na kumjulia hali, au kumwambia tu kuwa unampenda sana. Jitahidi sana kwa hili.
4. ZINGATIA MAMBO YA MSINGI.
Hapa jambo la msingi ni kuelewa kuwa jambo mnalolilenga ambalo ni ndoa linapaswa kuwaje, pia linataka mambo gani na ili lifanikiwe, linahitaji kuwa na vitu gani na hivyo kuanza kuyafanya hivyo vinavyohitajika. Tafakari kwa undani juu ya mafanikio ya mauhusiano yenu  na kuishi kuligana na misingi hiyo itakayowapelekea katika mahusiano wenye  mafanikio. Ishi kulingana na matazamio yatakayowaletea tofauti katika maisha  yenu.
5.CHUKUA HATUA.
Kamwe huwezi kumuongoza rafiki yako nmna anavyoweza kuishi kwenye uhusiano, lakini unaweza kuzuia mazingira hasi katika uhusiano. Unatakiwa kuchukua asilimia mia moja ya wajibu wako kwa namna unavyoenenda katika uhusiano. Pia amua kile unachokiamini na kukifanya kuwa cha kweli na kukifanya kuwa sahihi asilimia mia.
6. BADILI MITAZAMO HASI KUWA KATIKA ORODHA YA MAJUKUMU.
Baada ya kuanguka katika nyanja fulani fulani za mahusiano badili mitazamo na majibu yote hasi na kuwa katika mitazamo chanya. Kwa mfano kama hauna furaha na yule umpendaye inakupasa kutafuta na kuandaa orodha ya vitu utakamvyomfanyia mwenzi wako awe na furaha kwa hakika mkiwa pamoja nae.